Sunday, June 19, 2016

WENGER AKATA TAMAA NA VARDY.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amekiri Jamie Vardy anajipanga kukaa uhamisho wa kwenda katika klabu hiyo ili aweze kubakia Leicester City. Mshambuliaji huyo ambaye alitwaa taji la Ligi Kuu akiwa na Leicester msimu uliopita, mustakabali wake umekuwa ukijadiliwa sana baada ya Arsenal kutenga paundi milioni 20 ambazo zingeweza kutengua mkataba wake. Vardy mwenyewe alikataa kufanya uamuzi wowote wa uhamisho kwenda Emirates mpaka baada ya kumalizika kwa michuano ya Ulaya ili aweze kujipa muda wa kuweka mkazo katika michuano hiyo akiwa na Uingereza. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo, Wenger amesema Vardy bado ni mchezaji wa Leicester na anadhani ataamua kubakia katika klabu yake kwa msimu ujao.

No comments:

Post a Comment