Wednesday, July 20, 2016

ARSENAL YAMGEUKIA KOULIBALY.

BEKI wa Napoli, Kalidou Koulibaly anadaiwa kutolewa ofa na klabu kadhaa kubwa za Ulaya ikiwemo Arsenal. Nyota huyo wa kimataifa wa Senegal mwenye umri wa miaka 25, ambaye anawindwa pia na klabu za Ligi Kuu za Chelsea na Everton anadaiwa kuthaminishwa kwa kitita cha euro milioni 45 ambacho hakuna yeyote aliyefikia. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger yuko sokoni kiangazi hiki akitafuta beki wa kiwango cha juu na wakati Koulibaly akibakia kwenye orodha ya wachezaji wanaowahitaji hakuna ofa yeyote iliyotolewa mpaka sasa. Wenger anakaribia kukamilisha usajili wake wa tatu kiangazi hiki kufuatia Rob Holding kufaulu vipimo vya afya huku mambo binafsi yakitarajiwa kujadiliwa katika siku chahe hizi.

No comments:

Post a Comment