Wednesday, July 20, 2016

LEICESTER CITY YAMTIA KITANZI NAHODHA WAKE.

NAHODHA wa Leicester City Wes Morgan amesaini mkataba mpya ambao utamuweka katika klabu hiyo mpaka Juni mwaka 2019. Beki huyo mwenye umri wa miaka 32 amecheza kila dakika katika mechi za ligi msimu uliopita wakati Leicester ilipokwenda kutwaa taji la Ligi Kuu. Morgan alijiunga na Leicester akitokea Nottingham Forest Januari mwaka 2012 na mpaka ameishaichezea klabu hiyo mechi 182 za ligi. Akihojiwa na mtandao wa klabu hiyo, Morgan amesema amefurahishwa sana na hatua hiyo kwani kila mtu anafahamu jinsi anavyoipenda klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment