Wednesday, July 20, 2016

URENO YAMUONGEZA KOCHA WAKE MKATABA.

CHAMA cha Soka cha Ureno-FPF kimetangaza kumuongeza mkataba kocha Fernando Santos mpaka 2020 baada ya kukiongoza kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo kutwaa taji la michuano ya Ulaya mwaka huu. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 61, ambaye amekuwa akikinoa kikosi hicho toka Septemba mwaka 2014, aliiongoza Ureno kutwaa taji lake la kwanza kubwa la kimataifa pamoja na kucheza bila nyota wake Cristiano Ronaldo katika fainali dhidi ya wenyeji Ufaransa mapema mwezi huu. Mkataba wake mpya alioongezwa utamfanya kukiongoza kikosi hicho katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 na ile ya ijayo ya Ulaya. Santos amewahi kufundisha klabu kubwa nchini Ureno zikiwemo Benfica, Sporting Lisbon na Porto huku pia akiwahi kuinoa timu ya taifa ya Ugiriki.

No comments:

Post a Comment