Wednesday, July 20, 2016

POGBA ADAIWA KUOMBA KUONDOKA KWENDA UNITED.

VYOMBO vya habari nchini Italia vimeripoti kuwa Paul Pogba ameihabalisha Juventus kuwa anataka kuondoka katika klabu hiyo na kwenda kujiunga na Manchester United. Tetesi hizo zimekuja kufuatia madai kuwa makamu mwenyekiti wa United Ed Woodward ameikosa safari ya ziara ya China kwa ajili ya kuanzisha mazungumzo ya kumnasa kiungo huyo. Magazeti mbalimbali ya nchini Italia yamepamba kurasa zao na taarifa mbalimbali za kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa huku mengine yakienda na mbali na kudai kuwa tayari wameshaafikiana makubaliano na United. Gazeti lingine lilidai kuwa Pogba anatarajiwa kusaini mkataba mnono wa miaka mitano ambao utamfanya kupata mara mbili ya mshahara anaopata hivi sasa.

No comments:

Post a Comment