Wednesday, July 20, 2016

CONTE AMKOMALIA COSTA.

MENEJA mpya wa Chelsea, Antonio Conte amesema mshambuliaji wake Diego Costa ataendelea kubaki katika klabu hiyo msimu ujao na ni mchezaji muhimu katika mipango yake. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania, amekuwa akihusishwa na tetesi za kurejea katika klabu yake ya zamani ya Atletico Madrid. Costa mwenye umri wa miaka 27 amefunga mabao 36 katika mechi 77 alizocheza toka amejiunga na Chelsea mwaka 2014. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo, Conte amesema Costa atabakia nao kwani amekuwa akijituma na anafurahia kufanya kazi na wachezaji wenzake pamoja naye.

No comments:

Post a Comment