Wednesday, July 20, 2016

BA KUENDELEA KUCHEZA SOKA AKIPONA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Shanghai Shenghua Demba Ba amesisitiza hatastaafu soka pamoja na kupata majeruhi mabaya ya kuvunjika mguu katika mchezo wa Ligi Kuu ya China. Katika tukio hilo la kutisha lililotokea Jumapili iliyopita wakati wa mchezo wa derby ya Shanghai, Ba alipinga mguu vibaya mguu wake wa kushoto baada ya kukwatuliwa na beki w SIPG Sun Xiang wakati akijaribu kuwania mpira. Mara baada ya kuvunjika hofu ilizuka kuwa soka la Ba mwenye umri wa miaka 31 linaweza kukomea hapo, lakini mshambuliaji huyo wa zamani wa Chelsea, West ham United na Newcastle United amesema hana mpango wowote wa kutundika daruga zake. Akihojiwa Ba amesema anafahamu kuwa hayo ni majeruhi mabaya lakini anafahamu anaweza kuvuka mtihani huo hivyo hawezi kukata tamaa. Ba amesema msimu wa ligi ya huko unamalizika Novemba na mpya unaanza Machi hivyo atajitahidi kufanya kila awezalo ili aweze kupona kwa wakati tayari kwa msimu ujao.

No comments:

Post a Comment