Tuesday, July 19, 2016

MAN UNITED SASA WATENGA OFA YA KUFURU KWA POGBA.

KLABU ya Manchester United inadaiwa kutuma ofa ya mwisho ya euro milioni 125 kwa ajili ya kiungo wa kimataifa wa Ufaransa Paul Pogba. United chini ya meneja wake mpya Jose Mourinho wamekuwa wakihaha kumuwania nyota huyo na wako tayari kuvunja rekodi ya dunia ya usajili kwa ajili ya kiungo huyo wa Juventus. Dili la jumla linadaiwa kuwa litawagharimu United kiasi cha euro milioni 185, huku klabu hiyo ikiwa tayari kumpa ofa ya mkataba wa miaka mitano wenye thamani ya euro milioni 12 kwa kila msimu. Taarifa zinadai pia kuwa Pogba anatarajia kukunja asilimia 20 ya ada hiyo ya mauzo yake ambayo itakuwa kiasi cha euro milioni 25.

No comments:

Post a Comment