Tuesday, July 19, 2016

MADRID YAKARIBIA KUMNASA GOMES.

KLABU ya Real Madrid inadaiwa kukaribia kumsajili kiungo wa Valencia Andre Gomes kwa kitita cha euro milioni 50. Valencia wanadaiwa kutaka kwanza euro milioni 65 kwa ajili ya kiungo huyo mwenye umri wa miaka 22 lakini Madrid wao wanataka kulipa euro milioni 50 na zingine waje kumalizika baadae. Taarifa zinadai kuwa Zinedine Zidane anamuona nyota huyo wa kimataifa Ureno kama chaguo sahihi atakaeweza kubadilishana na Luka Modric. Manchester United, Chelsea na Barcelona nazo pia zinamuwania mchezaji huyo.

No comments:

Post a Comment