Tuesday, July 19, 2016

ARSENAL YANYATIA BEKI LA BOLTON.

KLABU ya Arsenal, inadaiwa kutenga ofa ya paundi milioni mbili kwa ajili ya beki wa Bolton Wanderers Rob Holding. Chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 20 ni zao kutoka katika shule ya soka ya Bolton na alikuwepo katika kikosi cha Uingereza cha vijana chini ya umri wa miaka 21 ambacho kilishinda taji la Toulon kiangazi hiki. Holding alishinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Bolton msimu uliopita baada ya kuibuka katika kikosi cha timu hiyo mwanzoni mwa msimu. Kwa upande mwungine, Wanderers wanafikiria kutoa ofa kwa beki wa zamani w Brighton Gordon Greer.


No comments:

Post a Comment