Tuesday, July 19, 2016

MARIO GOTZE ANUKIA DORTMUND.

OFISA mkuu wa Borussia Dortmund, Hans-Joachim Watzke amesema angefurahi kuona Mario Gotze akiichezea tena timu hiyo lakini amesisitiza hakuna dili lolote lililofanyika mpaka sasa na Bayern Munich. Mwenyekiti wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge alibainisha mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa klabu hizo mbili zipo katika mzungumzo ya kujadili uhamisho wa Gotze. Gotze mwenye umri wa miaka 24, alisababisha mtikisiko wakati alipoondoka Dortmund kwenda kujiunga na mahasimu woa wa Bundesliga Bayern mwaka 2013, lakini toka wakati huo ameshindwa kung’aa akiwa na mabingwa hao wa Ujerumani. Lakini pamoja na mazungumzo kuwa bado yanaendelea, Watzke amesisitiza kuwa bado safari ni ndefu kwa pande hizo mbili kufikia makubaliano. Watzke amesema pamoja na kuwa anatamani Gotze arejee tena Dortmund lakini mazungumzo bado yanaendelea na hakuna uamuzi wowote ulioafikiwa.

No comments:

Post a Comment