Tuesday, July 19, 2016

NITARUDI NIKIWA IMARA ZAIDI - RONALDO.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ameapa kurejea tena akiwa imara zaidi tayari kwa ajili ya msimu wa 2016-2017 baada ya kupata majeruhi ya goti katika michuano ya Ulaya mapema mwezi huu. Ronaldo huku akibubujikwa na machozi alitolewa nje kwa machela baada ya kupata majeruhi ya goti katika mchezo wa fainali ya michuano ya Ulaya ambao Ureno walishinda dhidi ya wenyeji Ufaransa jijini Paris. Nyota huyo aliumia katika kipindi cha kwanza kufuatia kukwatuliwa na kiungo wa Ufaransa Dimitri Payet huku taarifa zikidai kuwa anaweza kukosa mwanzo wa msimu wa La Liga na Madrid. Hata hivyo, Ronaldo alituma picha za video katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram akiwaondoa hofu mashabiki wake na kudai kuwa atarejea akiwa imara zaidi.

No comments:

Post a Comment