Tuesday, July 19, 2016

NEYMAR NJE TUZO ZA MCHEZAJI BORA WA ULAYA.

SHIRIKISHO la Soka la Ulaya-UEFA limetangaza majina ya wachezaji 10 watakaowania tuzo ya mchezaji bora wa Ulaya kwa msimu wa 2015-2016. Nafasi kubwa miongoni mwa majina hayo yaliyoteuliwa anapewa nyota wa kimataifa wa Ureno na klabu Real Madrid Cristiano Ronaldo ambaye mbali na kutwaa mataji mawili makubwa ya Ulaya kwa klabu na nchi yake lakini pia ndiye mfungaji bora wa bara hil msimu uliopita. Majina 10 yaliyoteuliwa yametolewa katika orodha ya wachezaji 37 walioteuliwa awali na shirikisho hilo kabla ya kupigiwa kura ya mchujo. Mbali na Ronaldo katika orodha hiyo lakini pia wapo Lionel Messi na Luis Suarez kutoka Barcelona, Gareth Bale, Toni Kroos na Pepe wote kutoka Madrid, Thomas Muller na Manuel Neuer kutoka Bayern Munich, Antonio Griezmann kutoka Atletico Madrid na Gianluigi Buffon kutoka Juventus.

No comments:

Post a Comment