Friday, July 15, 2016

EL CLASICO DESEMBA.

KLABU za Barcelona na Real Madrid zinatarajiwa kukutana Desemba katika ratiba mpya ya msimu wa 2016-2017 wa La Liga iliyotolewa leo. Madrid waliomaliza katika nafasi ya pili katika msimamo wa La Liga nyuma ya Barcelona msimu uliopita, watasafiri kwenda Camp Nou katika wikiendi ya Desemba 3 au 4 ukiwa ni mchezo wao wa mwisho kwa la Liga kabla ya kusafiri kwenda kushiriki michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia nchini Japan wakiwa kama mabingwa wa Ulaya. Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Desemba 8 na kumalizika Desemba 18 mwaka huu. Mechi ya marudiano kati ya mahasimu hao wa La Liga inatarajiwa kufanyika Santiago Berbabeu kati ya Aprili 22 au 23 mwakani.

No comments:

Post a Comment