Friday, July 15, 2016

RONALDO AMEUNGA MKONO UJIO WANGU LA LIGA - NANI.

WINGA mpya wa Valencia, Nani amesema mchezaji mwenzake wa Ureno Cristiano Ronaldo ameunga mkono hatua yake hiyo ya kwenda La Liga kufuatia mafanikio waliyopata katika michuano ya Ulaya. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29, amesaini mkataba wa miaka mitatu na Valencia akitokea Fenerbahce ya Uturuki kwa kitita cha euro milioni 8.5 ambapo alidumu kwa msimu mmoja baada ya kuondoka Manchester United. Nani alianza katika mechi zote saba na kufunga mabao matatu wakati Ureno ilipotwaa taji la Ulaya, huku rafiki yake na mchezaji mwenzake Ronaldo akimuunga mkono kupata mafanikio wakati atakapocheza soka kwa mara ya kwanza nchini Hispania. Winga huyo alitambulishwa mbele ya mashabiki 12,000 wa Valencia waliojitokeza Mestalla jana na anatarajiwa kushindana na Ronaldo pindi msimu wa la Liga utakapoanza. Akihojiwa Nani amesema Ronaldo alimpongeza na kumwambia kuwa Valencia ni klabu kubwa nchini humo na ataweza kuzoea haraka mazingira ya La Liga.

No comments:

Post a Comment