Friday, July 15, 2016

ROMA YAMTENGEA NACHO EURO MILIONI 15.

KLABU ya AS Roma inadaiwa kufikiria kutuma ofa ya euro milioni 15 kwa ajili ya kumuwania beki wa Real Madrid, Nacho. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26, amecheza mechi 22 msimu uliopita na kwasasa amekuwa chaguo la nne kwa Zinedine Zidane baada ya Sergio Ramos, Pepe na Raphael Varane. Kabla ya kurejea kwa maandalizi ya msimu mpya, Nacho alielezwa na Madrid kuwa bado wanamuhitaji, wakati mchezaji mwenyewe naye akipania kupigania nafasi yake. Lakini Zidane sasa anatarajiwa kukutana na beki huyo kuzungumzia mustakabali wake na uhamisho wake kwenda Roma utategemea na matokeo ya kikao hicho.

No comments:

Post a Comment