Wednesday, July 20, 2016

SHERIA KALI MPYA ZAWEKWA KUDHIBITI TABIA MBAYA KATIKA LIGI KUU.

MPANGO wa kupunguza tabia zisizovumilika kwa wachezaji na mameneja katika soka la Uingereza umetangwazwa rasmi leo. Katika taarifa iliyotolewa na Ligi Kuu, Ligi ya Soka ya Uingereza na Chama cha Soka cha nchi hiyo imedai kuwa maadili mabovu yamefikia hatua ya kutokubalika. Kuanzia msimu huu mpya wa ligi, kadi nyekundu zitaonyeshwa kw mchezaji atakayemfuata mwamuzi wa mchezo na kutumia lugha isiyokuwa sahihi au kumuonyesha ishara yeyote mbaya. Tabia katika maeneo ya benchi la ufundi pia nazo zitachukuliwa hatua kali. Mwenyekiti wa Ligi Kuu, Richard Scudamore amesema kumekuwa na wasiwasi kwa kipindi kirefu kuwa wachezaji wamekuwa wakivuka mipaka kwa tabia zao wanazoonyesha.

Makosa ambayo mchezaji anaweza kupewa kadi ya njano.
*Kuonyesha wazi kutomuheshimu mwamuzi wa mchezo,
*Kuonyesha shari kwa maamuzi yaliyotolewa
*Kumvaa mwamuzi uso kwa uso
*Kumkimbilia mwamuzi ili kupinga uamuzi uliotolewa
*Shambulizi, lugha ya matusi au ya kunyapaa na ishara ishara yeyote kumuelekea mwamuzi
*Kugusana na mwamuzi yeyote katika tukio ambalo sio la kumfanyia fujo
*kadi ya njano walau kwa mchezaji mmoja wakati wachezaji wawili au wa zaidi wa timu watakwenda kumzonga mwamuzi.

Makosa mapya ambayo mchezaji anaweza kupata kadi nyekundu ni*Kama mchezaji atamvamia mwamuzi na kumshambulia, kutumia lugha ya matusi au kunyapaa au kumnyooshea ishara ishara kwenda kwake
*Kugusana na mwamuzi wa mchezo kwa nia ya kumfanyia fujo au kupingana na uamuzi wake

No comments:

Post a Comment