Tuesday, August 23, 2016

AC MILAN YAITOLEA NJE CHELSEA KWA ROMANGNOLI.

KLABU ya AC Milan imethibitisha kukataa mazungumzo na Chelsea kwa ajili ya kumuwania beki wake Alessio Romagnoli. Klabu hiyo ya Serie A imedai Chelsea walitoa ofa ya euro milioni 35 kwa ajili ya nyota huyo wa kimataifa wa Italia mwenye umri wa miaka 21, lakini wamekataa ofa hiyo. Meneja mpya wa Chelsea emapania kuimarisha safu ya ulinzi ya Chelsea kabla ya kufungw akwa dirisha la usajili wa kiangazi baada ya kutofurahishwa na jinsi safu hiyo ilivyo sasa. Baada ya kuchemka kumsajili beki wa Napoli Kalidou Koulibaly, Chelsea waliamua kuhamishia nguvu zao kwa Romangnoli ambaye anafananishwa na nguli wa zamani wa Milan Alessandro Nesta.

No comments:

Post a Comment