Tuesday, August 23, 2016

NEWELL'S OLD BOYS NA MATUMAINI YA KUMSAJILI MESSI.

KLABU ya Newell’s Old Boys bado ina matumaini ya kumsajili Lionel Messi kutoka Barcelona baada ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018. Messi alianza soka lake katika klabu hiyo ya Argentina kabla ya kuhamia katika akademi maarufu ya soka ya Barcelona inayoitwa La Masia. Toka wakati huo nyota huyo amekwenda kutwaa tuzo nne za Ballon d’Or na kuwa mmoja wachezaji bora kabisa kuwahi kutokea katika soka. Makamu wa rais wa Newell’s Cristian D’Amico ana matumaini ya kuona mshambuliaji huyo akirejea tena katika Uwanja wa Marcelo Biesla katika siku zijazo.

No comments:

Post a Comment