Tuesday, August 23, 2016

NEYMAR APEWA LIKIZO ZAIDI.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Neymar anatarajiwa kukosa mchezo dhidi ya Athletic Bilbao mwishoni mwa wiki hii na hatarejea Hispania mpaka baada ya mapumziko kupisha mechi za kimataifa mwanzoni mwa Septemba. Baada ya kufunga penati ya ushindi dhidi ya Ujerumani na kuiwezesha Brazil kutwaa medali yake ya kwanza ya dhahabu ya Olimpiki Jumamosi iliyopita, nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 alitegemewa kurejea mazoezini kwenye klabu yake kesho. Hata hivyo, vyombo vya habari vya Hispania vimedai meneja wake Barcelona Luis Enrique amempa mapumziko nyota huyo ya kubakia Brazil mpaka Septemba. Neymar sasa anatarajiwa kurejea Catalonia kwa ajili ya mchezo wa Alaves ambao utafanyika Septemba 10 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment