Thursday, August 25, 2016

BRAVO ATUA RASMI MAN CITY, BYE BYE JOE HART.

KLABU ya Manchester City imefanikiwa kukamilisha rasmi usajili wa kipa Claudio Bravo kutoka Barcelona. Bravo mwenye umri wa miaka 33, amehamia Itihad kwa mkataba wa miaka minne akichukua nafasi ya Joe Hart, ambaye anategemewa kuondoka kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili kiangazi hiki. Meneja wa City Pep Guardiola alikuwa akitafuta kipa ambaye ana uwezo mkubwa wa kutumia miguu yake kuzuia mipira na sasa amempata. Bravo alijiunga na Barcelona akitokea Real Sociedad mwaka 2014 na kuwasaidia mabingwa hao wa Hispania kutwaa mataji mawili ya La Liga na moja la Ligo ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment