Tuesday, August 23, 2016

BRAVO ATUA UINGEREZA KUKAMILISHA UHAMISHO WAKE MAN CITY.

KIPA wa Barcelona, Claudio Bravo anadaiwa kutua nchini Uingereza mapema leo kwa ajili ya kukamilisha uhamisho wake kwenda Manchester City. Meneja wa City Pep Guardiola amemtaja Bravo kama kipa wake namba moja kwa msimu huu baada ya kuamua kumtema Joe Hart katika mipango yake. Taarifa zinadai kuwa Bravo atakaribia kulipwa mara ya mbili mshahara wake wa sasa wakati atakaposaini mkataba wake na City. Kipa huyo wa kimataifa wa Chile ambaye alishinda taji la Copa America akiwa na nchi yake mara mbili mfululizo katika miaka miwili iliyopita, alikuwa akilipwa euro milioni 3.5 na Barcelona lakini sasa anaweza kupata kiasi cha euro milioni sita kwa City.

No comments:

Post a Comment