Tuesday, August 23, 2016

PRINCE BOATENG AANZA KWA KISHINDO LAS PALMAS.

KIUNGO wa kimataifa wa Ghana, Kevin-Prince Boateng amefunga bao lake la kwanza La Liga katika ushindi wa mabao 4-2 iliyopata timu yake mpya ya Las Palmas dhidi ya Valencia huko Mestalla. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29, alijiunga na Las Palmas kwa mkataab wa mwaka mmoja mwezi huu akiwa kama mchezaji huru baada ya AC Milan kumtema. Boateng ameilipa Las Palmas kwa kuonyesha kuwa mchezaji muhimu wa kigeni kwa kufunga bao hilo katika dakika ya 31 ya mchezo. Mara baada ya mchezo huo nyota huyo aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter akieleza furaha yake ya kufunga mabao katika ligi zote nne kubwa alizowahi kucheza. Kabla ya kwenda Las Palmas, Boateng amewahi kucheza klabu za Hertha Berlin, Tottenham Hotspurs, Borussia Dortmund, Portmouth, Milan na Schalke.

No comments:

Post a Comment