Thursday, August 25, 2016

JOE HART AACHA KITENDAWILI CITY.

KIPA wa Manchester City, Joe Hart amesema kuisaidia timu hiyo kutinga hatua ya makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya katika mchezo ambao unaweza kuwa wa mwisho kwake kuitumikia klabu hiyo, ni jambo ya kipekee. Hart ambaye anategemewa kuondoka kufuatia Claudio Bravo kukaribia kukamilisha usajili wake, alikuwa akipigiwa kelele na mashabiki wakati wote wa mchezo huo wa marudiano ambao City ilishinda bao 1-0 dhidi ya Steaua Bucharest. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo ambao City walizonga mbele kwa jumla ya mabao 6-0, Hart amesema wana meneja bora ambaye atakuwa na mawazo tofauti katika maamuzi yake. Naye meneja wa City Pep Guardiola amesema anafahamu kuwa kipa huyo ni nguli katika klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment