Thursday, August 25, 2016

KOMBE LA LIGI: CITY VS SWANSEA, LEICESTER VS CHELSEA.

KLABU ya Manchester United inatarajiwa kupambana na timu ya League One ya Northampton Town katika mzunguko wa tatu wa michuano ya Kombe la Ligi wakati timu ya League Two ya Accrington Stanley wao wakiwa wageni wa West Ham United. Mabingwa watetezi wa michuano hiyo Manchester City wao watasafiri kuifuata Swansea City, huku Liverpool waliofungwa katika hatua ya fainali nao wakiwa wageni wa Derby Count. Mabingwa wa Ligi Kuu Leicester City wataikaribisha Chelsea, wakati Southampton nao wakiwa wenyeji wa Crystal Palace na Hull City wakiifuata Stoke City katika mechi zitakazokutanisha timu za Ligi Kuu. Kwa upande mwingine Arsenal wao watakuwa wageni wa Nottingham Forest huku Queens Park Rangers-QPR wakiikaribisha Sunderland. Mzunguko wa tatu wa michuano hiyo unataajiwa kuchezwa wiki inayoanzia Septemba 19 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment