Monday, August 29, 2016

EMERY AJIPA MOYO PAMOJA NA KIPIGO.

MENEJA wa Paris Saint-Germain-PSG, Unai Emery amedai ana uhakika kikosi chake kitajifunza kutokana na uzoefu wa mechi zao za ugenini baada ya kupata kipigo cha kushtukiza kutoka kwa AS Monaco jana. Katika mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Louis II, PSG walitandikwa mabao 3-1 na mahasimu wao Monaco. Matokeo yanamaanisha PSG imeshuka mpaka nafasi ya tano katika msimamo wa Ligue 1, kufuatia kuanza msimu kwa ushindi. Akihojia Emery amesema walianza mchezo huo vyema lakini baada ya Monaco kuwafunga bao la kuongoza hali ilibadilika kwani walifanikiwa kuulinda ushindi wao vyema. Hata hivyo, Emery anaamini wachezaji wake wamejifunza kutokana na mchezo huo na watafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza.

No comments:

Post a Comment