Monday, August 29, 2016

MOURINHO KUMPA MAPUMZIKO ZAIDI IBRAHIMOVIC.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amesema Zlatan Ibrahimovic atapewa mapumziko zaidi kupisha mechi za kimataifa. Mshambuliaji huyo ameanza vyema msimu na klabu hiyo kwa kufunga bao katika mechi ya ngao ya hisani na baadae mabao mengine matatu katika mechi tatu za Ligi Kuu. Kufuatia kustaafu kuitumikia Sweden baada ya michuano ya Ulaya mwaka huu, nyota huyo hatakuwa na majukumu ya kimataifa mwishoni mwa wiki ijayo, lakini Mourinho bado anataka kumlinda zaidi. Akihojiwa Mourinho amesema ukiwa na umri wa miaka 34 huwezi kucheza mechi 70 kwa msimu hivyo ameapa wachezaji wengine ambao hawajachaguliwa na timu zao za taifa siku mbili za mapumziko huku Ibrahimovic akimpa siku nne.

No comments:

Post a Comment