Monday, August 29, 2016

MUSTAFI AKIRI OZIL ALIMSHAWISHI KWENDA ARSENAL.

BEKI wa kimataifa wa Ujerumani, Shkodran Mustafi amebainisha kuomba ushauri kutoka kwa nyota wa Arsenal Mesut Ozil kuelekea uhamisho wake wa kwenda Emirates. Mustafi anatarajiwa kuthibitishwa rasmi kuwa mchezaji wa Arsenal wiki hii baada ya meneja Arsene Wenger kutangaza kuwa kilichobaki na kusaini mkataba ili kukamilisha uhamisho wake kutoka Valencia. Mustafi ambaye pia amewahi kucheza katika klabu ya Everton atakuwa akicheza sambamba na Mjerumani mwenzake Per Mertesacker katika safu ya ulinzi ya Arsenal. Akihojiwa Mustafi amesema hajaonana na Mertesacker kwa kipindi kirefu kwasababu alishastaafu soka la kimataifa lakini amekuwa akizungumza na Ozil na kumwambia kila anachohitaji kuhusu Arsenal. Mustafi aliendelea kudai kuwa kila kitua lichoambiwa kilimvutia hivyo haikuwa kazi kwake kukubali kujiunga nao kwani siku zote amekuwa akiipenda klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment