Wednesday, August 17, 2016

MAHREZ ASAINI MIAKA MINNE LEICESTER.

KLABU ya Leicester City imetangaza kuwa winga wao Riyad Mahrez amesaini mkataba mpya wa miaka minne na mabingwa hao wa Ligi Kuu. Mahrez mwenye umri wa miaka 25, amekuwa akihusishwa na tetesi za kuwindwa na Arsenal katika kipindi hiki cha usajili wa kiangazi. Lakini nyota huyo wa kimataifa wa Algeria amefuata nyayo za mshambuliaji Jamie Vardy kwa kusaini mkataba wa muda mrefu na klabu hiyo. Mahrez amefunga mabao 17 na kusaidia mengine 11 ambayo yaliisaidia kwa kiasi kikubwa Leicester kutwaa ubingwa msimu uliopita. Akihojiwa Mahrez amesema Ligi Kuu ni ligi nzuri na anataka kubaki hapo kwa kipindi kirefu iwezekanavyo.

No comments:

Post a Comment