Wednesday, August 17, 2016

POGBA FITI KUIVAA SOUTHAMPTON.

KIUNGO mpya wa Manchester United, Paul Pogba anatarajiwa Ijumaa hii kuichezea kwa mara ya kwanza timu hiyo katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Southampton. Nyota huyo ambaye aliondoka kwa mlango wa nyuma mwaka 2012 kwenda Juventus kabla ya kurejea kwa ada ya paundi milioni 89 iliyovunja rekodi ya dunia, alishindwa kuanza katika mchezo uliopita dhidi ya Bournemouth kwasababu ya kutumikia adhabu ya mechi moja aliyotoka nayo Italia. Akihojiwa kuhusu mchezo wa kesho, Pogba amesema anajisikia yuko fiti na amekuwa akifanya mazoezi kwa siku 10 lakini itategemea meneja wake Jose Mourinho atakavyoona inafaa. Pogba aliendelea kudai kuwa ameshazoea hali hiyo kwani amekuwa akifanya mazoezi hata wakati alipokuwa likizo hivyo anajiona yuko sawa.

No comments:

Post a Comment