Monday, August 22, 2016

NEYMAR AJIVUA UNAHODHA BRAZIL.

MSHAMBULIAJI nyota wa Brazil, Neymar amesema anatarajia kuachia beji yake ya unahodha baada ya kufunga penati ya ushindi dhidi ya Ujerumani na kuipatia nchi yake medali ya kwanza ya dhahabu katika Olimpiki. Nyota huyo wa Barcelona aliteuliwa kuwa nahodha na Dunga katika michuano ya Kombe la Dunia ambayo walifungwa katika hatua ya nusu fainali na Ujerumani kw amabao 7-1, mchezo ambao Neymar aliukosa kwasababu ya majeruhi. Baada ya ushindi huo, Neymar amesema tayari ameshakuwa bingwa na ameamua kuachia beji yake ya unahodha kwani ametimiza kile alichokuwa kikiota wakati wote. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa anaivua beji hiyo ili kutoa nafasi kwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Brazil Tite kuchagua nahodha atakayemuhitaji.

No comments:

Post a Comment