Saturday, August 27, 2016

PALERMO YATUMA OFA KWA BALOTELLI.

MAKAMU wa rais wa klabu ya Palermo na Italia, Guglielmo Micciche amesema wametuma ofa Liverpool kwa ajili ya Mario Balotelli na sasa wanasubiri kusikia kama ofa yao itakubaliwa. Balotelli ameondolewa kabisa katika mipango ya Liverpool na kuna uwezekano mkubwa wa kuondoka kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wiki ijayo. Akihojiwa Micceche amesema anafahamu ni jambo gumu lakini wameamua kujaribu kumuwania mshambuliaji huo. Micceche aliendelea kudai kuwa tayari wameshatuma ofa hivyo kazi imebaki kwa Liverpool waikubali au waikatae.

No comments:

Post a Comment