Saturday, August 27, 2016

PSG YAKOMAA NA MATUIDI.

KLABU ya Paris Saint-Germain-PSG inajipanga kukataa ofa za kumuwania Blaise Matuidi kwa kumsainisha mkataba mpya kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 amekuwa akihusishwa na tetesi za kuwindwa na Juventus katika siku za karibuni. Hata hivyo, rais wa PSG Nasser Al Khelaifi ametupilia mbali tetesi hizo na kudai kuwa Matuidi anataka kubakia hapo na anatarajiwa kupewa mkataba mpya. Al Khelaifi alikaririwa na gazeti moja nchini Ufaransa akithibitisha kuwa nyota huyo hatauzwa kipindi hiki cha kiangazi. Matuidi alijiunga na PSG akitokea St Etienne mwaka 2011 na katika kipindi chote cha miaka minne wameshinda taji la Ligue 1.

No comments:

Post a Comment