Saturday, August 27, 2016

PELLEGRINI ATIMKIA CHINA.

MENEJA wa zamani wa Manchester City, Manuel Pellegrini amejiunga na klabu ya Hebei China Fortune inayoshiriki Ligi Kuu ya China. City waliziba nafasi ya Pellegrini mwenye umri wa miaka 62 kwa kumchukua Pep Guardiola Juni mwaka huu pamoja na meneja huyo raia wa Chile kuwapa taji la Ligi Kuu mwaka 2014. Pellegrini anaungana na makocha wengine wenye majina makubwa waliokwenda China akiwemo Sven-Goran Eriksson na Luis Felipe Scolari. Kikosi cha Hebei kinawajumuisha nyota wa kimataifa wa Argentina Ezequiel Lavezzi, mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Gervinho na chipukizi wa zamani wa Chelsea Gael Kakuta. Klabu hiyo kwasasa inashikilia nafasi ya saba katika msimamo wa ligi huku kukiwa kumebaki michezo saba kabla ya msimu kumalizika.

No comments:

Post a Comment