Wednesday, September 28, 2016

ALLARDYCE AIACHA UINGEEREZA HUKU AKISIKITIKA.

ALIYEKUWA kocha wa timu ya taifa ya Uingereza, Sam Allardyce amesema amesikitishwa kuacha kibarua chake hicho baada ya kukitumikia kwa siku 67 pekee. Hatua hiyo imekuja baada ya gazeti moja nchini humo kutoa taarifa za uchunguzi wao kuwa, kocha huyo alitoa ushauri wa jinsi gani ya kukwepa mkono wa sheria katika suala la usajili. Allardyce aliomba radhi kutokana na hilo na kudai kuwa anafahamu kuwa baadhi ya kauli zake alizotoa huko nyuma zimesababisha aibu kubwa. Chama cha Soka cha Uingereza-FA kimeseam kauli ya kocha huyo sio ya kimaadili na kuongeza kuwa wameamua kusitisha mkataba wake kwa maelewano. Gareth Southgate sasa ndio amepewa mikoba ya muda kuingoza timu hiyo katika mechi zao nne zijazo, wakati mchakati mwingine ukifanyika.

No comments:

Post a Comment