Wednesday, September 28, 2016

TEVEZ KUSTAAFU MWISHONI MWA MWAKA HUU.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Argentina, Carlos Tevez amelaumu vyombo vya habari kwa adhabu aliyopewa na kuongeza kuwa anaweza kuachana na soka itakapofika mwishoni mwa mwaka huu. Tevez mwenye umri wa miaka 32, ambaye kwasasa anacheza katika klabu ya nyumbani kwao ya Boca Juniors, alicheza kwa mafanikio barani Ulaya katika klabu za Manchester United, Manchester City na Juventus. Lakini nyota huyo ameeleza hisia zake kwa mambo kadhaa yanayotokea katika ligi ya nyumbani ikiwemo shinikizo kubwa lililowekwa kwa Boca na vyombo vya habari ambavyo amevilaumu kw akufungiw akwake mechi tatu. Akihojiwa Tevez amesema adhabu aliyopewa kwa kukosoa ni kama imetoka kwa waandishi na sio katika kamati. Tevez pia aliponda utaratibu wa upangaji ratiba fupifupi katika soka la nchi hiyo na kuongeza kuwa ni moja ya mambo ambayo yanamfanya afikirie kustaafu soka mwishoni mwa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment