Wednesday, September 28, 2016

VARDY AELEZA KULICHOMFANYA KUIKACHA ARSENAL.


MSHAMBULIAJI nyota wa Leicester City, Jamie Vardy amesema alikataa ofa ya kujiunga na Arsenal majira ya kiangazi ili ajaribu na kujenga mafanikio waliyopata kwa kutwaa taji la Ligi Kuu. Inadaiwa kuwa nyota huyo alikaribia kujiunga na Arsenal kufuatia klabu hiyo kutengua kitenzi katika mkataba wake cha paundi milioni 20, lakini Vardy mwenyewe alibadili maamuzi yake na kuamua kubakia King Power. Akihojiwa Vardy amesema kikubwa kilichombakisha Leicester sio uaminifu bali alitaka kuendelea kujenga kile walichokifanya na wachezaji wenzake. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa Leicester ni klabu inayokua na anafurahia kuwa sehemu ya makuzi ya klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment