Wednesday, September 28, 2016

SARE ZA MADRID ZAMCHANGANYA ZIDANE.

MENEJA wa Real Madrid, Zinedine Zidane amesema anahisi kukosa bahati baada ya timu yake kuruhusu bao la kusawazisha dakika za mwishoni jana na kupelekea kupata sare ya mabao 2-2 katika mchezo wao wa kundi F wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Dortmund. Katika mchezo huo Madrid walianza kuongoza kwa bao safi la kushtukiza la Cristiano Ronaldo kabla ya Dortmund hawajasawazisha kupitia kwa Pierre-Emerick Aubameyang aliyetumia vyema makosa yaliyofanywa na Keylor Navas. Madrid waliongeza bao lingine kupitia kwa Raphael Varane katikati ya kipindi cha pili lakini walishindwa kulinda ushindi huo baada ya Christian Pulisic aliyeingia akitokea benchi kusawazisha zikiwa zimebaki dakika tatu. Sare hiyo waliyopata jana Madrid inakuwa ya tatu baada ya zile mbili walizopata katika La Liga dhidi ya Villarreal na Las Palmas. Akihojiwa Zidane amesema anadhani wanakosa bahati kwani wanacheza vizuri na bidii lakini mwishoni wanashindwa kuzuia ushindi wanaokuwa nao.

No comments:

Post a Comment