Wednesday, September 28, 2016

FA SASA KUMGEUKIA WENGER BAADA YA KUONDOKA ALLARDYCE.

CHAMA cha Soka cha Uingereza-FA kinadaiwa kuwa kitajaribu kumuwania kocha wa Arsenal, Arsene Wenger mwishoni mwa msimu huu ili awe kocha mpya wa timu ya taifa ya nchi hiyo. Sam Allardyce aliachia wadhifa wake kama kocha wa nchi hiyo jana, ikiwa zimepita siku 67 toka alipoteuliwa kushika nafasi hiyo na kukiacha kikosi hicho kikitafuta kocha mpya. Wenger ambaye anasheherekea miaka 20 akiwa na klabu hiyo, anapewa nafasi kubwa kuchukua nafasi hiyo huku FA wakidaiwa kuwa tayari walishamfuata kabla ya kumchagua Allardyce. Hata hivyo, Arsenal haitarajiwi kumuachia kirahisi meneja wao huyo wa muda mrefu na mmiliki wa timu hiyo Stan Kroenke bado ana matumaini kuwa atakubali kuongeza mkataba.

No comments:

Post a Comment