Tuesday, September 27, 2016

KLOPP ATAKA TIMU YAKE KUIMARIKA ZAIDI.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema bado kuna nafasi ya kuimarika kama kikosi chake kinataka kupigania taji la Ligi Kuu msimu huu pamoja na kuanza vyema kampeni zao. Liverpool ambao mara ya mwisho kutwaa la ligi ilikuwa mwaka 1990, waliirarua Hull City kwa mabao 5-1 Jumamosi iliyopita na kukwea mpaka nafasi nne katika msimamo, wakiwa nyuma ya vinara Manchester City kwa alama tano. Liverpool wameshinda mechi ngumu za ugenini dhidi ya Arsenal na Chelsea huku wakiwababua mabingwa Leicester City kwa mabao 4-1 msimu huu, na mechi pekee waliyopoteza ni ile waliyofungwa na Burnley. Akihojiwa Klopp amesema ni kweli kwasasa wanacheza vizuri lakini bdo kuna nafasi ya kuimarika ili waweze kuendeleza wimbi lao la ushindi.

No comments:

Post a Comment