Tuesday, September 27, 2016

WENGER AMTETEA ALLARDYCE KUFUATIA KASHFA INAYOMKABILI.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kocha wa timu ya taifa ya Uingereza Sam Allardyce anahitaji kupewa nafasi ya kujitetea, kufuatia tuhuma zilizotolewa na gazetini. Uchunguzi wa gazeti la Daily Telegraph unadaiwa kung’amua kuwa Allardyce mwenye umri wa miaka 61 alitumia nafasi yake kufanya mazungumzo ya dili la paundi 400,000 na kutoa ofa ya ushauri wa jinsi gani wanaweza kukwepa sheria katika usajili wa mchezaji. Meneja huyo wa zamani wa Bolton Wanderers, Newcastle United na West Bromwich Albion pia amedaiwa kukikosoa Chama cha Soka cha Uingereza-FA, meneja aliyeondoka Roy Hodgson na msaidizi wake wa zamani Gary Neville. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo, Wenger amesema Allardyce anatakiwa kupewa nafasi ya kujitetea na matumani yake ni kwamba ataweza kusafisha jina lake. Allardyce mwenyewe bado hajajibu chochote kuhusiana na tuhuma hizo na amekuwa na mkutano na mwenyekiti wa FA Greg Clarke pamoja na ofisa mkuu Martin Glenn leo.

No comments:

Post a Comment