Tuesday, September 27, 2016

YAYA TOURE AIPONDA FIFA.

KIUNGO wa Manchester City, Yaya Toure amesema wachezaji na mashabiki wanaweza kuumia kufuatia hatua ya Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kuvunja kikosi kazi kilichoundwa kwa ajili ya kupambana na vitendo vya kibaguzi katika soka. Toure mwenye umri wa miaka 33, alikuwa mmoja wa wajumbe wa kikosi kazi hicho kilichoundwa mwaka 2013 kusaidia kutokomeza ubaguzi. Katibu mkuu wa FIFA, Fatma Samba Diouf Samoura amesema kikosi kazi hicho kilikuwa na kazi maalumu ambayo tayari wameimaliza. Hata hivyo, hatua hiyo imekosolewa vikali na wadau mbalimbali, akiwemo Toure ambaye alifanyiwa vitendo vya kibaguzi na mashabiki wa CSKA Moscow Octoba mwaka 2013. Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ivory Coast amesema hatua hiyo ya FIFA itaweza kuwaumiza mashabiki na wachezaji kama mipango sahihi isipowekwa.

No comments:

Post a Comment