Tuesday, September 27, 2016

ZIDANE AKANUSHA KUWEPO MPASUKO KATI YAKE NA RONALDO.

MENEJA wa Real Madrid, Zinedine Zidane amepuuza tetesi kuwa kuwa kuna mpasuko kati yake na Cristiano Ronaldo kuelekea mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Dortmund baadae leo. Zidane amedai kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Ureno ni mtu mwenye uelewa mzuri wa kujua kocha hufanya maamuzi kwa faida ya timu. Ronaldo amefunga mabao mawili katika mechi nne alizocheza msimu huu, likiwemo bao zuri la mpira wa adhabu alilofunga katika mchezo wao wa ufunguzi walioshinda mabao 2-1 dhidi ya Sporting Lisbon. Wakati alipotolewa mapema katika sare ya mabao 2-2 waliyopata dhidi ya Las Palmas, nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 alionyesha kukasirika. Hata hivyo, Zidane amesema kila kitu kikosi sawa katika kambi yao na sio jambo la kushangaza kwa mchezaji kuchukia akitolewa kwani hutokea mara kwa mara na sio kwa Ronaldo peke yake.

No comments:

Post a Comment