Tuesday, September 27, 2016

MO FARAH AAKA KUINOA ARSENAL.

MWANARIADHA nyota wa Uingereza na bingwa mara nne wa Olimpiki, Mo Farah amesema angependa kuja kuwa mwalimu wa mazoezi wa klabu ya Arsenal. Farah amekuwa shabiki wa Arsenal toka akiwa kijana mdogo na amesema yuko tayari kufanya kazi katika klabu hiyo inayotoka Kaskazini mwa London katika siku za usoni. Akihojiwa Farah ambaye ni mzaliwa wa Somalia amesema kitu kimoja anchokipenda kwa dhati ni soka na amekuwa na mahusiano mazuri na Arsenal. Farah aliendelea kudai kuwa alianza kuishabikia Arsenal toka alipowasili nchini Uingereza kwa mara ya kwanza akiwa mdogo kwasababu alipenda wanavyocheza. Kitu kingine kilichomvutia Farah ni kuwepo kwa wachezaji wengi wenye asili ya Afrika na siku moja angependa kuja kufanya nao kazi.

No comments:

Post a Comment