Tuesday, September 27, 2016

BARCELONA IKO POA BILA MESSI - ENRIQUE.

MENEJA wa Barcelona, Luis Enrique amesema wana wachezaji wa kutosha ambao wanaweza kuziba pengo liliachwa na nyota wao Lionel Messi. Messi anatarajiwa kuukosa mchezo wa huo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Monchengladbach utakaofanyika kesho kutokana na majeruhi ya nyonga. Jumamosi iliyopita Barcelona walionesha wanaweza kusonga mbele bila Messi baada ya kuitandika Sporting Gijon kwa mabao 5-0 katika mchezo wa La Liga. Barcelona wamefunga mabao 18 katika mechi nne toka walipotandikwa mabao 2-1 nyumbani na Alaves Septemba 10 mwaka huu huku Neymar na Luis Suarez wakiwa katika kiwnago kizuri. Akihojiwa Enrique amesema ana wachezaji wa kutosha ambao wanaweza kuicheza vyema na kuziba pengo la Messi ambaye anatarajiwa kukaa nje kwa kipindi cha wiki tatu.

No comments:

Post a Comment