Monday, September 26, 2016

NYOTA WA PARAGUAY AZITOA UDENDA KLABU ZA LIGI KUU.

KLABU za Swansea City na Sunderland zinadaiwa kuingia katika kinyang’anyiro cha kuwania saini ya Federico Santander. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Paraguay ambaye kwasasa anakipiga katika klabu ya Fc Copenhagen ya Denmark, atakuwa akitazamwa na maskauti wa klabu zote mbili katika mchezo wao wa Jumanne dhidi ya Club Brugge. Santander amefunga mabao sita katika mechi 17 kwenye mashindano yote msimu huu na anaweza kuvutiwa kuhamia Ligi Kuu. Taarifa pia zinadai Everton na Olympique Lyon nazo ni klabu zingine zinazomfuatilia kwa karibu mshambuliaji huyo.

No comments:

Post a Comment