Monday, September 26, 2016

MWENYEKITI WA BOURNEMOUTH AKANUSHA ARSENAL KUMTAKA MENEJA WAO.

MWENYEKITI wa Bournemouth, Jeff Mostyn amekanusha Arsenal kumfuata meneja wao Eddie Howe.  Meneja huyo wa Bournemouth amekuwa akihusishwa na tetesi za kuchukua mikoba ya Arsene Wenger msimu ujao kufuatia meneja huyo raia wa Ufaransa kumalizika mkataba mkataba wake kiangazi mwakani. Lakini Mostyn anaamini Howe bado ana mambo mengi ya kufanya katika Uwanja wa Vitality wakati klabu hiyo ikijaribu kujiimarisha katika Ligi Kuu. Akihojiwa Mostyn amesema ni jambo la fahari kuona meneja wao akitafutwa na klabu zingine ingawa hakuna yeyote aliyewasiliana nao rasmi kuhusu suala hilo. Mwenyekiti huyo aliendelea kudai kuwa bado wana kazi kubwa ya kufanya na Howe kwani wanahitaji kuimarisha klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment