Monday, September 26, 2016

WABAGUZI KUKIONA - FIFA.

KATIBU mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Fatma Samoura amekingia kifua kikosi kazi cha kupambana na masuala ya ubaguzi akidai kuwa mpango imara unatarajiwa kuwekwa ili kutokomeza kabisa hali hiyo. Kumezuka wasiwasi juu ya uamuzi wa wa kubadilisha kikosi kazi hicho huku ikiwa imebaki miaka miwili kabla ya michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Urusi mwaka 2018. Lakini Samoura ambaye alikuwa akizungumza jijini Manchester amesisitiza kuwa pamoja na mabadiliko hayo bado kutakuwa na sera isiyoruhusu kabisa aina yeyote ya unyanyapaa kwa kikosi kazi kipya kutakachopewa majukumu hayo. Samoura amesema kikosi kazi kipya kitakachopewa kazi hiyo kitakuwa imara zaidi ya ilivyokuwa mara ya kwanza kwani wamepanga kutokomeza kabisa masuala yeyote ya unyanyapaa katika soka.

No comments:

Post a Comment