Tuesday, September 20, 2016

BALE, RONALDO WAREJEA KIKOSI CHA MADRID.

MENEJA wa Real Madrid, Zinedine Zidane amethibitisha kuwa Cristiano Ronaldo na Gareth Bale watakuwepo katika dhidi ya Villarreal utakaochezwa kesho. Nyota hao wawili walikosa mchezo wa Jumapili iliyopita dhidi ya Espanyol kutokana na majeruhi na maradhi. Hata hivyo, haikuwadhuru sana Madrid kwani walishinda mchezo huo kwa mabao 2-0 yaliyofungwa na James Rodriguez na Karim Benzema na kuendeleza rekodi yao nzuri ya ushindi. Akihojiwa kuelekea katika mchezo huo, Zidane amesema Bale na Ronaldo wako tayari hivyo atawatumia katika kikosi chake. Hata hivyo, Madrid watamkosa beki wao Pepe ambaye hakufanya mazoezi leo lakini mabeki wengine wanne waliobakia wako fiti.

No comments:

Post a Comment