Friday, September 23, 2016

KUFA NA KUPONA LIGI YA MABINGWA AFRIKA.

MICHUANO ya Ligi ya Mabingwa Afrika inatarajiwa kuendelea tena mwishoni mwa wiki hii kwa timu nne kutafuta nafasi ya kutinga fainali ya michuano hiyo. Katika nusu fainali ya kwanza Zamalek ya Misri itakuwa kama inaenda kukamilisha ratiba itakapokwenda kukwaana na Wydad Casablanca ya Morocco kwa katika mechi ya mkondo wa kwanza mabingwa hao mara tano walishinda kwa mabao 4-0. Kama Wydad wakifanikiwa kuifunga Zamalek na kutinga fainali itakuwa timu ya kwanza kufanya hivyo baada ya kupita miaka 52 wakati timu ya Hafia ya Guinea ilipotoka nyuma ikiwa imefungwa mabao 3-0 na Asec Mimosas ya Ivory Coast na kuja kulipiza kisasi nyumbani kwa kushinda mabao 5-0 mwaka 1976. Katika nusu fainali nyingine Zesco United ya Zambia wataifuata Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini huku wakiwa kifua mbele kwa ushindi wa mabao 2-1 waliopata katika mchezo wao wa mkondo wa kwanza. Mechi zote mbili za marudiano zitachezwa kesho ambapo Sundowns wataikaribisha Zesco jijini Pretoria na Wydad wakipepetana na Zamalek jijini Rabat.

No comments:

Post a Comment